Usiri wa London katika kutangaza idadi ya watoto wa Afghanistan waliouawa kinyama na jeshi la Uingereza

BBC imeripoti kuwa takriban watoto 64 wa Afghanistan waliuawa katika operesheni za jeshi la Uingereza wakati wa miaka ya vita nchini Afghanistan, ambapo serikali ya nchi hii hapo awali ilikuwa imekubali kesi 16 tu.

Vyombo vya habari vya Uingereza vilitangaza kuwa, watoto wasiopungua 64 waliuawa katika operesheni za jeshi la nchi hiyo nchini Afghanistan kuanzia mwaka 2006 hadi 2014.

Kulingana na BBC, kabla ya hili, serikali ya Uingereza ilikuwa imetambua vifo vya watoto 16 tu kutoka Afghanistan.

Vyombo hivi vya habari vya Uingereza vimeandika kuwa serikali tayari imeweka fidia kwa watoto 64 wa Afghanistan, ambayo ni mara 3 ya idadi iliyokuwa imetangaza rasmi hapo awali.

Wengi wa watoto hawa walikufa wakati wa shambulio la anga na katikati ya moto wa vikosi vya Uingereza.

Ripoti hii ilitolewa na serikali ya nchi hii kwa ombi la shirika la misaada la Uingereza liitwalo Action for War-related Violence (AOAV).

Shirika hili la hisani pia lilisema kuwa idadi ya raia waliouawa na jeshi la Uingereza nchini Afghanistan ni kubwa kuliko ilivyotangazwa hadi sasa.

Kulingana na taasisi hii, idadi ya watoto waliouawa katika vita nchini Afghanistan huenda ikaongezeka hadi 135.

Hapo awali, BBC ilichapisha ripoti kuhusu uhalifu wa kivita wa vikosi maalum vya Uingereza wakati wa vita vya NATO nchini Afghanistan.

Kwa mujibu wa utafiti wa mtandao huu wa Uingereza, maajenti maalum wa jeshi la Uingereza “SAS” wakati wa vita nchini Afghanistan mara nyingi waliwaua wafungwa na watu wasio na silaha na kufanya uhalifu wa kivita katika nchi hii.

BBC iliripoti kwamba vikosi maalum vya Uingereza viliwaua wafungwa 54 na kuwazuilia raia kinyume cha sheria wakati wa operesheni ya usiku mnamo 2010.

Gulbdin Hekmatyar, Kiongozi wa Chama cha Kiislamu cha Afghanistan pia amejibu jinai za kivita za askari wa Uingereza na kusema kuwa, Mahakama ya The Hague inapaswa kuchunguza jinai za kivita za askari wa Uingereza na vikosi vya kigeni nchini Afghanistan na kuwafungulia mashtaka wahusika.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *