Swala ya Isha na Tarawehe katika Msikiti wa Al-Aqsa usiku wa tarehe 21 Ramadhani

Makumi ya maelfu ya Wapalestina wanaendelea kufanya ibada na itikaf katika Msikiti wa Al-Aqsa katika Jerusalem inayokaliwa kwa mabavu licha ya vizuizi vinavyopo, vilivyowekwa na vikosi vya kizayuni.

Vyanzo vya habari vya ndani vilitangaza kuwa raia wa Palestina walifungua mfungo wao baada ya Swala ya Maghrib katika viwanja vya Msikiti wa Al-Aqswa na kuswali Isha na Tarawehe (Swala za Jamaa za Sunnah baada ya Swala ya Maghrib hasa nyakati za usiku wa Ramadhani) msikitini humo.

Licha ya vikwazo vilivyowekwa na wavamizi hao, maelfu ya Wapalestina walikusanyika kwa ajili ya swala katika Msikiti wa Al-Aqsa.
Licha ya mashambulizi ya walowezi wa Kiyahudi na kuvunjiwa heshima Msikiti wa Al-Aqswa, taifa la Palestina halijarudi nyuma katika kukabiliana na makazi na Uyahudi wa maeneo matukufu na linaendelea kutekeleza itikafu katika Msikiti wa Al-Aqswa katika siku zilizosalia ndani ya mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya “Hamas” iliwaita umati wa watu wa Palestina katika uhamasishaji wa jumla wa kuswali swala na itikafu za kila siku katika Msikiti wa Al-Aqsa na kuutetea.
Harakati hii iliwatahadharisha wavamizi hao kujiepusha na upumbavu na vitendo vyovyote dhidi ya Msikiti wa Al-Aqswa na usalama wa waumini waliomo ndani yake, na kusisitiza kuwa, kuvunja utukufu wa msikiti huu ni tishio kwa usalama na amani ya eneo na mashambulizi dhidi ya imani. ya Waislamu wote.

Harakati hii ilizitaka nchi za Kiarabu na Kiislamu na mashirika ya kimataifa kuchukua jukumu la kusimamisha uchokozi wa wavamizi na serikali yao ya kifashisti kwenye Msikiti wa Al-Aqsa.

Siku ya Ijumaa asubuhi, mamia ya walowezi wenye itikadi kali waliushambulia Msikiti wa Al-Aqsa chini ya uungaji mkono mkubwa wa vikosi vya utawala ghasibu vya Kizayuni.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *