Wanawake nchini Kenya wafanya sherehe ya giza katika siku ya wapendanao

Mamia ya wanawake wa Kenya wafanya sherehe ya giza ya wapendanao kukomesha mauaji ya wanawake nchini.

Huku watu ulimwenguni wakisherehekea Siku ya Wapendanao kwa maua na chokoleti, wanawake wa Kenya wakiwa katika maombolezo wakiwa wamevalia nguo nyeusi na kuwasha mishumaa na kushikilia waridi jekundu katika hafla ya kuwaenzi wanawake zaidi ya 30 waliouawa nchini humo ndani ya mwaka wa 2024.
Madhumuni ya hafla hiyo ni kuishinikiza serikali ya Kenya kushughulikia matakwa ya vuguvugu la mauaji ya wanawake, ambayo ni pamoja na kutangaza mauaji ya wanawake na unyanyasaji dhidi ya wanawake kuwa jambo la kitaifa na kuunda tume ya kutokomeza vyote viwili.
Waandalizi wanasema walipanga hafla hiyo katika Siku ya Wapendanao ili kuvutia “uhalisia wa giza” wa ukatili wa kijinsia na wanawake kuuawa na wale wanaowapenda.
Kauli ya wanawake wa Kenya siku ya wapendanao
Wanawake wa Kenya katika taarifa ya vuguvugu hili walisema: “Hasara mbaya ya wanawake kuuawa na wenzi wao au wanafamilia; Imekuwa vichwa vya habari vya vyombo vya habari.

Takwimu kutoka Kituo cha Takwimu cha Afrika zinaonyesha kuwa waume na wapenzi – sio wageni – wanahusika na theluthi mbili ya mauaji ya wanawake nchini Kenya.
Maandamano hayo yanafuatia maandamano ya nchi nzima mwezi Januari ambapo Wakenya 20,000 walishiriki, wakitaka serikali ichukue hatua kuzuia na kushtaki kesi za unyanyasaji wa kingono na kijinsia na mauaji ya wanawake, ambayo wanasema mara nyingi hupuuzwa.

 

 

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *