Mlipuko mjini Kabul wasababsha kifo cha mashahidi 20
Vyanzo vya habari vya Afghanistan viliripoti mlipuko katika msikiti mmoja katika mji wa Kabul. Kulingana na mwandishi wa tovuti ya Afghanistan ya shirika la habari la Fars, vyanzo vya habari vya Afghanistan viliripoti mlipuko huo huko Kabul. Wakaazi wa eneo la Khairkhaneh katika mji wa Kabul wanasema kuwa mlipuko ulitokea katika msikiti wa “Sadiqiyeh” dakika…
Iraq katika mkondo wa kushtadi zaidi mkwamo wa kisiasa
Uamuzi wa makundi na mirengo ya kisiasa ya Iraq wa kufanya mikusanyiko ya barabarani umeifanya anga ya kisiasa ya nchi hiyo kuwa tete zaidi na mkwamo wa kisiasa unaoikabili nchi hiyo kushtadi zaidi. Iraq imeendelea kushuhudia mkwamo wa kisiasa kwa miezi kumi sasa ambao chimbuko lake ni matokeo ya uchaguzi wa Bunge uliofanyika Oktoba mwaka…
Wapalestina wafichua njama ya Israel ya kuubomoa kikamilifu msikiti wa Al Aqsa
Duru za Palestina katika mji wa Baitul Muqaddas (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu zimefichua njama ya awamu tatu iliyoandaliwa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kwa lengo la kuubomoa msikiti mtukufu wa Al Aqsa. Kwa mujibu wa duru hizo, lengo la njama hiyo ni kuchimba misingi kwa madhumuni ya kuzifanya kuta za msikiti wa Al…
HAMAS: Muqawama una uungaji mkono mkubwa wa Wapalestina wa Ukingo wa Magharibi
Kiongozi mmoja mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiisalamu ya Palestina HAMAS amesema kuwa, muqawama uko chini ya mwavuli wa uungaji mkono wa kivitendo wa Wapalestina na jambo hilo ndilo linalozidi kutia nguvu harakati za muqawama katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Kituo cha upashaji habari cha Palestina kimeripoti habari hiyo na kunukuu matamshi…
Mwanamke Saudia afungwa jela miaka 34 kwa ujumbe wa Twitter
Saudi Arabia imemhukumu mwanamke mmoja kifungo cha miaka 34 jela, eti kwa kupatikana na hatia ya kumiliki ukurasa wa Twitter na kusambaza ujumbe unaoukosoa utawala wa Aal-Saud kupitia mtandao huo wa kijamii. Salma al-Shehab, 34, mama wa watoto wawili wadogo na mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Leeds alikamatwa na vyombo vya usalama vya Saudia Januari…
Wapalestina wa Gaza wataka kushtakiwa Wazayuni walioua watoto wao
Wakazi wa Ukanda wa Gaza wamefanya maandamano wakitaka kufunguliwa mashitaka utawala wa Kizayuni wa Israel katika mahakama za kimataifa, kwa kuua watoto wa Kipalestina katika eneo hilo ambalo liko chini mzingiro. Wakazi wa Gaza, familia na jamaa za watoto wa Kipalestina waliouawa shahidi katika mashambulizi ya hivi karibuni ya jeshi katili la utawala haramu wa…
Wanajeshi wa mwisho wa Ufaransa waondoka Mali
Mabaki ya wanajeshi wa Ufaransa waliondoka nchini Mali jana Jumatatu, kuashiria mwisho wa Operesheni ya Barkhane katika nchi hiyo ya eneo la Sahel barani Afrika. Taarifa ya Vikosi vya Jeshi la Ufaransa imesema, askari wa mwisho wa kikosi cha Barkhane waliokuwa katika ardhi ya Mali wameondoka na kuvuka mpaka baina ya nchi hiyo na Niger….
Karzai: Wananchi wa Afghanistan wametaabika mno kwa kuweko majeshi ya Marekani nchini kwao
Hamid Karzai Rais wa zamani wa Afghanistan amesema kuwa, wananchi wa nchi hiyo wamedhurika pakubwa katika kipindi cha miaka 20 iliyopita ya kuweko majeshi ya kigeni yakiwemo ya Marekani katika nchi yao. Karzai amesema hayo katika mahojiano maalumu aliyofanyiwa na chombo kimoja cha habari cha India ambapo sambamba na kuzungumzia matukio ya mwaka mmoja uliopita…