Magaidi 50 wa Daesh wahamishiwa Iraq kutoka nchini Syria
Kitengo cha upashaji habari cha jeshi la Iraq kimetoa ripoti rasmi na kusema kuwa karibu wanachama 50 wa genge la kigaidi na ukufurishaji la Dashe (ISIS) wamehamishiwa mkoani Nainawa (Nineveh) Iraq kutoka katika kambi ya al Hawl ya nchini Syria. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, hivi sasa kuna takriban wakazi 56,000 katika kambi ya…
Wamagharibi wakosolewa kwa undumakuwili juu ya vita Ukraine na Gaza
Harakati inayopinga dhulma na ukandamizaji wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina imekosoa vikali undumakuwili wa nchi za Magharibi kuhusu vita nchini Ukraine kwa upande mmoja na katika Ukanda wa Gaza, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu kwa upande mwingine. Harakati ya Kimataifa ya Kuususia Utawala haramu wa Israel BDS katika taarifa jana Jumamosi…
Nyayo za mafia Waisraeli katika madai ya Wizara ya Sheria ya Marekani dhidi ya IRGC
Wizara ya Sheria ya Marekani imechapisha taarifa inayodai kuwa mtu mmoja kwa jina Shahram Poursafi, ambaye wizara hiyo ilimtaja kuwa mwanachama wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), alipanga kumtumia Mmarekani mmoja kumuua John Bolton na afisa mwingine wa utawala wa Donald Trump. Madhumuni ya njama hiyo imetajwa kuwa ni kulipiza kisasi…
Ghalibaf: Muqawama wa Palestina umetoa bishara ya kuangamia utawala wa Kizayuni
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, muqawama na mapambano ya harakati ya Jihad al Islami ya Palestina mbele ya utawala wa Kizayuni wa Israel yametoa bishara njema ya kuangamia utawala huo pandikizi. Shirika la habari la IRNA limemnkuu Mohammad Bagher Ghalibaf akisema hayo leo katika kikao cha wazi cha Bunge…
Wanamichezo Wairaq wakataa kupambana na timu ya Israel katika mashindano ya Romania
Wanamichezo wawili Wairaqi wa mchezo wa tenisi wamekataa kupambana na wanamichezo kutoka utawala haramu wa Kizayuni wa Israel katika michuano ya Paralampiki inayofanyika nchini Romania. Wanamichezo wengi wanaounga mkono Palestina katika nchi za Kiislamu na Kiarabu hawautambui utawala wa Kizayuni na hawako tayari kupambana na wapinzani wao wanaowakilisha Israel katika mashindano mbalimbali ya michezo. Tovuti…
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuhusu kuinuliwa hadhi ya Harakati ya Jihad Islami
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amejibu barua ya Katibu Mkuu wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina na kusema, “mapambano (muqawama) ya kishujaa ya Jihad Islami yatapelekea kupanda hadhi ya harakati hiyo katika mapambano sambamba na kusambaratisha hadaa za utawala wa Kizayuni na kuufedhehesha utawala huo.” Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi…
HAMAS yapongeza misimamo ya waziri wa ulinzi wa Pakistan dhidi ya Israel
Msemaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amepongeza msimamo thabiti ulioonyeshwa na waziri wa ulinzi wa Pakistan dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel. Waziri wa ulinzi wa Pakistan Khawaja Muhammad Asef ameieleza serikali ya Uingereza na waziri wa mambo ya nje wa nchi hiyo kuwa Azimio la Balfour la mwaka…
Athari za mashambulio ya Yemen zinaendelea, Wakuwait wakatazwa kutumia drone Imarati
Athari za mashambulio ya kulipiza kisasi na ya kujihami ya wananchi wa Yemen dhidi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) bado zingalipo na sasa serikali ya Kuwait imewataka wananchi wake wasitumie ndege yoyote isiyo na rubani wanapokuwa nchini Imarati, ili wasije wakajiingiza kwenye matatizo. Baada ya Umoja wa Falme za Kiarabu kufanya jinai kubwa…