
Putin aliamuru jeshi la Urusi kuingia mashariki mwa Ukraine
Ikulu ya Kremlin imetangaza kuwa rais wa Urusi ameitaka Wizara ya Ulinzi ya Urusi kutia saini makubaliano na mikoa ya Donetsk na Luhansk iliyoko mashariki mwa Ukraine ili kutuma wanajeshi kulinda amani katika maeneo hayo. Kwa mujibu wa Huduma ya Kimataifa ya Shirika la Habari la Fars, baada ya uamuzi wa Rais wa Urusi Vladimir…

Hizbullah : Tumeonyesha sehemu ndogo tu ya uwezo wa kivita tuloinao
Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon, Hizbullah imesema imeonyesha sehemu ndogo tu ya uwezo wake wa kivita ambao umeushtua na kuudhalilisha utawala wa Kizayuni wa Israel. Mwenyekiti wa ‘Mrengeo wa Muqawama’ (Mapambano ya Kiislamu)’ ambao ni tawi la kisiasa la Hizbullah katika Bunge la Lebanon amesema mafanikio ya ndege isiyo na rubani au drone…

Mali imeitaka Ufaransa kuwaondoa askari wake walioko nchini haraka iwezekanavyo
Serikali ya mpito ya Mali imeitaka Ufaransa kuwaondoa bila kuchelewa askari wake wa operesheni Barkhane na Takuba nchini Mali. Takwa hilo la Mali linakuja masaa machache tu baada ya tangazo la Rais Emmanuel Macron na washirika wake la kuwaondoa askari wa nchi zao kutoka Mali katika miezi michache ijayo. Akitangaza uamuzi huo kupitia televisheni ya…

Je, Israel itaweza kuilinda Imarati dhidi ya ndege zisizo na rubani na makombora ya vikosi vya Yemen?
Wayemen wamesisitiza mara kwa mara kwamba vita vya muungano wa Saudia na Imarati dhidi ya Yemen katika kipindi cha miaka saba iliyopita kiuhakika ni vita vya Israel na Marekani, na kwamba tawala hizi mbili za Kiarabu na baadhi ya mamluki wengine wa kanda ya Kiarabu ni maonyesho tu ya vita hivi. Sisitizo la ajabu la…

Uteketezaji wa Bendera za Israel nchini Bahrain, hatua ya kulaani safari ya Bennett
Faraan : Waandamanaji wenye hasira nchini Bahrain wameteketeza kwa moto bendera za utawala wa Kizayuni wa Israel wakilaani safari ya siku mbili ya Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel, Naftali Bennet katika nchi hiyo ndogo ya Ghuba ya Uajemi. Maandamano yamefanyika kote katika nchi hiyo huku waandamanaji wakikanyaga bendera za Israel na kuziteketeza huku wakiwa…

Ali Khamenei : Uongozi wa Muqawama Asia Magharibi wayakata makali majigambo ya ubeberu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, muqawama unaokua na kuzidi kupata nguvu katika eneo la Asia Magharibi umesambaratisha kiburi na majigambo ya ubeberu. Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema hayo leo sambamba na kukaribia kumbukumbu ya harakati ya kihistoria ya wananchi wa Tabriz ya 29 Bahman 1356 Hijria Shamshia (18 Februari 1978) wakati alipozungumza kwa…

Muungano vamizi wazidi kushambulia mji mkuu Sana’a na miji mingine
Muungano vamizi unaoongozwa na Saudia na Imarati unaendelea kufanya jinai dhidi ya wananchi wasio na ulinzi wa nchi ya Kiarabu ya Yemen. Tangu mwezi Machi 2015 hadi hivi sasa, kila siku wananchi wasio na hatia wa Yemen wanamiminiwa mabomu na makombora na wavamizi wa nchi yao wanaoongozwa na Saudi Arabia na Umoja wa Falme za…

Nablos: Wapalestima 165 wajeruhiwa na wanajeshi wa Israel
Shirika la Hilal Nyekundu la Palestina limeripoti kuwa, Wapalestina wasiopungua 165 wamejeruiwa na wanajeshi makatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel mjini Nablos, katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan jana Ijumaa pekee. Kila siku Wazayuni wanaua na kujeruhiwa makumi ya Wapalestina pamoja na kuvunja nyumba zao, kuharibu mashamba yao na kuteka maeneo yao. Mamia…