Mchezaji tenisi ya mezani Mlebanon agoma kucheza na Mzayuni; aiunga mkono Palestina
Nyota chipukizi wa mchezo wa tenisi ya mezani raia wa Lebanon amejiondoa katika mashindano ya Kombe la Dunia ya Tenisi ya Mezani Kwa vijana Chipukizi (WTT) baada ya kupangwa kumenyana na mchezaji kutoka Israel (Palestina inayokaliwa kwa mabavu). Bissan Chiri binti wa miaka 11 kutoka Lebanon amekataa kucheza na mchezaji Mzayuni na kutangaza kuliunga mkono…
Walowezi wa Kizayuni wayateketeza kwa moto magari ya Wapalestina
Huku walowezi wa Kizayuni wakiendeleza hujuma zao dhidi ya raia wa Palestina, waliyateketeza kwa moto magari kadhaa ya Wapalestina katika mkoa wa Quds unaokaliwa kwa mabavu. Mapema ya Ijumaa hii walowezi wa Kizayuni walichoma moto magari kadhaa ya Wapalestina katika vijiji viwili vya Abu Ghosh na Ain Naquba katika mkoa wa Quds unaokaliwa kwa mabavu….
Utawala dhalimu wa Israel umebomoa zaidi ya skuli 50 za Wapalestina katika mwaka huu
Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa na Umoja wa Mataifa, utawala haramu wa Kizayuni wa Israel umebomoa zaidi ya skuli 50 za Wapalestina katika mwaka huu wa 2022. Ili kufikia malengo yao ya kujipanua, Wazayuni huvamia kila siku maeneo tofauti ya Palestina na kuwaua shahidi, kuwajeruhi au kuwatia nguvuni Wapalestina wasio na hatia. Kuhusiana na suala hilo,…
Mzayuni: Tusijidanganye, Waarabu hawaupendi utawala wa Kizayuni
Vyombo vya habari vya Kizayuni vimetuma timu kadhaa za waandishi na wataalamu wa vyombo vya habari kwenye Kombe la Dunia nchini Qatar; Miongoni mwa waandishi hao ni “Ohad Ben Hamo,” mwandishi wa habari wa Israel ambaye anajulikana kuwa ni mtaalamu wa masuala ya Waarabu na Wapalestina. Ben Hamo, ambaye anaelewa vizuri lugha ya Kiarabu, ni…
Polisi ya utawala wa Kizayuni yatangaza hali ya hatari baada ya miripuko ya al Quds
Polisi ya utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza hali ya hatari katika ardhi zote zinazokaliwa kwa mabavu ikihofia uwezekano wa wana muqawama wa Palestina kuekeleza tena oparesheni dhidi ya Wazayuni. Utawala wa Kizayuni wa Israel umetangaza hali hiyo ya hatari katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu ambapo vyombo vya habari jana asubuhi viliripoti kujiri miripuko miwili…
Mashabiki wa soka waendelea kuiunga mkono Palestina katika Kombe la Dunia
Mashabiki wa soka wanaoshuhudia fainalii za mashindano ya kandanda ya Kombe la Dunia nchini Qatar wameendelea kuonyesha himaya na uungaji mkono wao kwa taifa la Palestina. Mashabiki wa soka wa mataifa mbalimbali wameonekana wakiingia viwanjani kushuhudia mechi mbalimbali za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini Qatar wakiwa wamebeba bendera ya Palestina. Katika mechi iliyochezwa jana ya…
Sera ya machafuko ya Tel Aviv nchini Ukraine; Mafanikio ya Wazayuni kutokana na vita hayakuwa ila migogoro
Tovuti ya mtandao wa Al-Mayadeen katika ripoti yake sambamba na kuashiria kushindwa kwa sera za kigeni za utawala wa Kizayuni katika mgogoro wa Ukraine, imesisitiza kuwa, Tel Aviv haijapata mafanikio yoyote zaidi ya mzozo baina ya pande zote mbili za vita. Katika ripoti ya uchambuzi, tovuti ya mtandao wa “Al-Mayadeen” imezungumzia kushindwa kwa sera za…
Vyombo vya habari vya Kizayuni: Waarabu wanajitenga na sisi wakati wa Kombe la Dunia na wanapinga fikra ya uhalalishaji wa mapenzi ya jinsia moja
Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni vimesema kuwa, wakaazi wa nchi za Kiarabu duniani wanajiweka kando na sisi na wako kinyume na uhalalishaji wa mapenzi ya jinsia moja. Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni viliripoti jana (Jumanne, Novemba 22) kwamba mashabiki wanaozungumza lugha ya Kiarabu walijitenga na vyombo vya habari vya lugha ya…