Israel inadai kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar ameuawa

Israel inasema kua Sinwar aliuawa siku ya Jumatano kusini mwa Gaza. Israel inasema vikosi vyake vimemuua kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar huko Gaza.

“Baada ya kukamilisha mchakato wa kutambua mwili, tumeweza kuthibitishwa kuwa Yahya Sinwar hayupo tena,” jeshi la Israeli lilisema.

“Operesheni nyingi zilizofanywa na [jeshi la Israeli] na ISA [Shin Bet, ambayo ni huduma ya usalama ya ndani ya Israeli,] katika kipindi cha mwaka jana na katika wiki za hivi karibuni katika eneo ambalo ‘aliuliwa’ zilizuia harakati za uendeshaji za Yahya Sinwar kama alivyokuwa akifuatwa na majeshi na kupelekea kuondolewa kwake.”

Hamas haijatoa maoni yoyote kuhusu madai hayo ya Israel.

Israel imekuwa ikiendesha vita dhidi ya Gaza tangu Oktoba mwaka jana, na kuua zaidi ya Wapalestina 42,000, wengi wao wakiwa raia. Hilo lilifuatia mashambulizi yaliyoongozwa na Hamas kusini mwa Israel, ambapo watu 1,139 waliuawa.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *