Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, utawala wa Saudi Arabia unawazuia baadhi ya Waislamu kutekeleza ibada ya Hija kwa sababu ya misimamo ya kisiasa ya ukoo wa Aal Saud au misimamo ya Marekani na Israel dhidi ya Waislamu hao.
Sayyid Abdul Malik Badruddin al-Houthi ametoa pongezi kwa Umma wa Kiislamu, mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu na taifa la Yemen kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Adh’ha.
Al-Houthi amesema: Utawala wa Saudi unawakaribisha wajumbe wa Kiyahudi na Wazayuni kwa mikono miwili, tofauti kabisa na unavyozikaribisha jumbe za Waislamu.
Al-Houthi ameashiria vikwazo vya utawala wa Saudia kwa mahujaji na jinsi unavyowatoza ada kubwa mno na kusema: Saudi Arabia unatekeleza sera zinazokwamisha utekelezwaji wa ibada hiyo na unawaumiza mahujaji wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu kwa gharama nzito za kifedha kiasi kwamba Hija imekuwa mchakato mgumu.
Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema kuwa, gharama kubwa za kifedha kwa mahujaji ni usaliti wa kikatili na hazina uhalali wowote.
Amesema Saudi Arabia ilizuia ibada ya Hija kwa mahujaji kutoka nje ya nchi kwa kipindi cha miaka miwili kwa kisingizio cha maambukizi ya corona lakini wakati huo huo iliruhusu hafla za anasana na ufuska kufanyika nchini humo na kusahilisha safari za wageni kuingia Saudia.
Kiongozi wa Ansarullah amesema, Idi ya Adh’ha ni tukio kubwa la kuimarisha misingi ya Kiislamu, kusimama kidete katika njia ya haki na kujitolea kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Amesisitiza kuwa, sikukuu hii ni hafla ya kuimarisha mfungamano na upendo baina ya waumini, kuwafariji watu masikini, kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumuadhimisha Yeye SW,