Madai ya Netanyahu: Shirika la nyuklia limejisalimisha kwa Iran

Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, ambaye ndiye mkuu wa juhudi za kuzitia kisiasa shughuli za wakala wa nyuklia dhidi ya Iran, aliishutumu jumuiya hiyo ya kimataifa kwa kufanya siasa dhidi ya Iran katika baadhi ya matamshi ya siku ya Ijumaa.

Binyamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala huo ambao katika miaka ya nyuma umekuwa moja ya taathira kuu katika siasa za Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki kuelekea Iran, aliishutumu jumuiya hiyo ya kimataifa kwa kujisalimisha kwa Iran na kufanya siasa.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, Benjamin Netanyahu alidai kuwa IAEA inakabiliwa na hatari ya kuwa shirika la kisiasa na lisilo na umuhimu.

Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki, katika ripoti yake ya robo mwaka iliyochapishwa Jumanne wiki jana, lilithibitisha kufungwa kwa kesi kadhaa za madai dhidi ya Iran.

Pamoja na mambo mengine, shirika hilo limesema katika ripoti hiyo kwamba maelezo ya Iran kuhusu madai ya kuwepo kwa asilimia 84 ya chembechembe za uranium katika eneo la Iran hayaendani na tathmini zilizofanywa na wakaguzi wa shirika hilo la kimataifa.

Sehemu ya ripoti hiyo inasema: “Wakala huo uliiarifu Iran kwamba baada ya kutathmini data hiyo, ilifikia hitimisho kwamba maelezo yaliyotolewa hayaendani na maelezo ya Iran, na shirika hilo halina maswali zaidi katika suala hili katika hatua hii. ”

Katika ripoti hii, pia inaelezwa kuwa shirika hilo limefunga uchunguzi wake kuhusu ugunduzi wa uranium yenye asili ya binadamu huko Marivan. Duru za karibu na utawala wa Kizayuni zimedai mara kwa mara kwamba Marivan ni moja ya maeneo ya siri ya nyuklia ya Iran ambayo yanafanya kazi ya kutengeneza silaha.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilisema kuwa chembechembe za uranium zilizopatikana zinaweza kuwa zinahusiana na “zana na vifaa vya maabara” vinavyotumiwa na wachimbaji katika eneo hilo. Wakala wa nyuklia uliita jibu la Iran “maelezo yanayowezekana”.

Ripoti hiyo inasema: “Shirika hilo kwa sasa halina maswali zaidi kuhusu chembechembe za uranium zilizopungua zilizopatikana huko Marivan, na suala hili si miongoni mwa masuala yaliyosalia katika hatua hii.”

Siku ya Ijumaa, Netanyahu alisema katika taarifa yake kwa wajumbe wa baraza la mawaziri ambayo ilitangazwa kwenye televisheni ya utawala huo kuwa: “Iran inaendelea kusema uongo kwa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki.”

Ameongeza kuwa: “Iwapo chombo hicho kitakuwa shirika la kisiasa, majukumu yake ya ufuatiliaji nchini Iran pamoja na ripoti zake kuhusu shughuli za nyuklia za Iran hazitakuwa na umuhimu.”

Katika miaka ya hivi karibuni nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na utawala wa Kizayuni ziliituhumu Iran kwa kufuata malengo ya kijeshi katika mpango wa nyuklia wa nchi hiyo. Iran imekanusha vikali madai haya.

Iran inasisitiza kuwa ikiwa ni miongoni mwa nchi zilizotia saini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Nyuklia (NPT) na mwanachama wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, ina haki ya kupata teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani.

Aidha wakaguzi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki wametembelea vituo vya nyuklia vya Iran mara nyingi lakini hawajawahi kupata ushahidi wowote kwamba mpango wa amani wa nishati ya nyuklia nchini humo umeelekezwa kwenye malengo ya kijeshi.

Aidha, mwaka 2015, Iran ilifikia makubaliano na nchi zinazojulikana kama kundi la 5+1 ili kutatua mvutano kuhusu mpango wake wa nyuklia. Licha ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki kukiri kwa Iran kufuata majukumu yake yote, serikali ya Marekani ilijiondoa kwa upande mmoja katika makubaliano haya mwezi Mei 2017.

Katika upande mwingine utawala wa Kizayuni ndio pekee unaoshikilia silaha za nyuklia katika eneo la Asia Magharibi na kwa uungaji mkono wa Marekani umeweka mbali na ufuatiliaji wa kimataifa mpango wake wa silaha za nyuklia.

Mamlaka za utawala wa Kizayuni zilikuwa tayari zimeitikia ripoti hiyo mpya ya robo mwaka ya shirika hilo. Siku tatu zilizopita, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya utawala huu, “Liver Hayat”, pia alilaani kusitishwa kwa uchunguzi wa wakala wa atomiki kwenye kituo cha Marivan na kuelezea kuwa “suala la wasiwasi mkubwa” kwa Tel Aviv.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *