Rais wa FIFA apongeza timu za Afrika katika Kombe la Dunia

Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino amepongeza matokeo ya timu za Afrika katika michuano ya Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini Qatar baada ya timu ya Morocco kuweka historia na kufuzu kwa nusu fainali ya michuano hiyo ikiwa timu ya kwanza ya taifa kutokea katika bara la Afrika kuwahi kuvuka hatua ya robo fainali.

Morocco sasa imekuwa timu ya kwanza ya Afrika kushika nafasi ya nne katika Kombe la Dunia baada ya mechi yake ya jana na Croatia ambapo Croatia ilishinda kwa mabao mawili kwa moja.

“Nadhani Morocco ilicheza vizuri sana – walikuwa na mafanikio makubwa na walifanya kazi vizuri sana,” rais wa FIFA amesema.

 “Walicheza kwa hamu kubwa, dhamira na ubora usiopingika. Kufika fainali za Kombe la Dunia hakuwezi kufanyika kwa bahati. Ni matokeo ya juhudi za muda mrefu, uwekezaji wa shirikisho la soka la Morocco, wafanyakazi wote wa kiufundi, na kocha kijana wa Morocco ambaye pia amekuwa katika soka ya klabu nchini.”

Kombe la Dunia la mwaka huu nchini Qatar limebadilisha dhana potovu ya kandanda ya Afrika. Timu za taifa za Afrika zimejidhihirisha kuwa wapinzani wa nguvu baada ya wawakilishi wawili kati ya watano wa bara hilo Morocco na Senegal kutinga hatua ya mtoano kwa mara ya pili pekee katika historia.

Wakati huo huo, mataifa mengine matatu ya Afrika, Ghana, Cameroon, na Tunisia, hayakuondoka kwenye mashindano ya Qatar bila mapambano makali.

Rais wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) Gianni Infantino amepongeza matokeo ya timu za Afrika katika michuano ya Kombe la Dunia la FIFA 2022 nchini Qatar baada ya timu ya Morocco kuweka historia na kufuzu kwa nusu fainali ya michuano hiyo ikiwa timu ya kwanza ya taifa kutokea katika bara la Afrika kuwahi kuvuka hatua ya robo fainali.

Morocco sasa imekuwa timu ya kwanza ya Afrika kushika nafasi ya nne katika Kombe la Dunia baada ya mechi yake ya jana na Croatia ambapo Croatia ilishinda kwa mabao mawili kwa moja.

“Nadhani Morocco ilicheza vizuri sana – walikuwa na mafanikio makubwa na walifanya kazi vizuri sana,” rais wa FIFA amesema.

 “Walicheza kwa hamu kubwa, dhamira na ubora usiopingika. Kufika fainali za Kombe la Dunia hakuwezi kufanyika kwa bahati. Ni matokeo ya juhudi za muda mrefu, uwekezaji wa shirikisho la soka la Morocco, wafanyakazi wote wa kiufundi, na kocha kijana wa Morocco ambaye pia amekuwa katika soka ya klabu nchini.”

Kombe la Dunia la mwaka huu nchini Qatar limebadilisha dhana potovu ya kandanda ya Afrika. Timu za taifa za Afrika zimejidhihirisha kuwa wapinzani wa nguvu baada ya wawakilishi wawili kati ya watano wa bara hilo Morocco na Senegal kutinga hatua ya mtoano kwa mara ya pili pekee katika historia.

Wakati huo huo, mataifa mengine matatu ya Afrika, Ghana, Cameroon, na Tunisia, hayakuondoka kwenye mashindano ya Qatar bila mapambano makali.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *