Kundi la Freedom Action lilitangaza kuwa mahakama ya Al Saud ilimhukumu mwanaharakati wa haki za binadamu Salmi al-Shahab kifungo cha miaka 34 jela.
Kwa mujibu wa kundi hilo lenye makao yake makuu mjini Washington, al-Shahab, mama wa watoto wawili, alikuwa akiishi Uingereza na alikamatwa akiwa safarini kuelekea nchini mwake.
Akiwa Mshia, kila mara alitweet kuhusu sababu ya Palestina, haki za wanawake nchini Saudi Arabia na ulazima wa kuwaachia huru wafungwa wa fikra.