
Marekani yafumbia macho ukweli kuhusu mauaji ya Shireen Abu Akleh
Licha ya kuwepo ushahidi na dalili za wazi kuhusu mauaji ya Shireen Abu Akleh, mwandishi ya televisheni ya al-Jazeera ya nchini Qata, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetoa taarifa ikidai kwamba mauaji hayo hayakuwa ya makusudi. Hii ni katika hali ambayo mauaji hayo yalitekelezwa mbele ya macho ya mamilioni ya walimwengu na bila…

Familia ya Shireen yakosoa ripoti ya Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani
Watu wa familia ya Shireen Abu Akleh, mwandishi habari Mpalestina ambaye aliuliwa shahidi kwa kupigwa risasi na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel akiripoti matukio yaliyokuwa yakijiri katika mji wa Jenin, wamokosoa vikali ripoti iliyotolewa na Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani kuhusu mauaji hayo. Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani imetangaza…

Maandamano Marekani baada ya polisi kumuua kijana Mwafrika-Mmarekani
Maelfu ya waandamanaji waliokuwa na hasira waliingia barabarani katika jimbo la Ohio, katikati mwa Marekani siku ya Jumapili kulaani kitendo cha polisi kumuua kikatili kijana mwenye asili ya Kiafrika ambaye hakuwa na silaha. Maandamano hayo yameitishwa baada ya kusambaa klipu za video zinazoonyesha uhalifu huo wa kishetani. Klipu hizo za kuogofya zilionyesha maafisa wanane wa…

Mshauri wa Rais wa Iran: Magaidi wa ISIS wametokana na fikra za Kimarekani
Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kaumu na waliowachache kidini amesema kundi la kigaidi la ISIS au Daesh limetokana na fikra za Kimarekani. Kwa mujibu wa taarifa ya IRNA, Mamusta Abdulsalam Karimi Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika masuala ya kaumu na waliowachache kidini aliyasema…

Mbunge Marekani alaani nchi hiyo kujiingiza katika vita Ukraine kuvuna faida
Mjumbe mwanamke wa chama cha Republican katika Kongresi ya Marekani amekosoa vikali hatua ya Washington ya kuipa Ukraine msaada mkubwa wa kijeshi na kuisaidia nchi hiyo katika kile alichokiita vita vya niaba dhidi ya Russia. Mbunge huyo wa Georgia, Marjorie Taylor Greene amesema hayo katika ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter na kueleza kuwa:…

Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kuhusu jinai za Marekani
Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa ujumbe wa Twitter kwa mnasaba wa kukumbuka jinai ya meli ya kivita ya Marekani iliyotungua ndege ya abiria ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Ghuba ya Uajemi. Ujumbe huo umeambataisha taarifa za jinai hiyo ya kuogofya na kuwaenzi waliouawa shahidi katika tukio…

Siasa za kundumakuwili za Wamagharibi katika mgogoro wa Ukraine
Vita vya Ukraine vimeingia katika mwezi wake wa tano. Siasa za kundumakuwili za Wamagharibi kuhusu mgogoro huo hadi sasa zimesababisha mdororo mkubwa wa uchumi, ungezeko kubwa la umasikini katika mamilioni ya familia duniani, vifo vya makumi ya watu na vilevile kusababisha mamilioni ya watu huko Ukraine kuwa wakimbizi. Kupungua akiba ya mafuta ya kimkakati ya…

Ilhan Omar: Minnesota ina machafuko makubwa zaidi kuliko kambi ya wakimbizi Wasomali ya Dadaab
Mbunge Muislamu mwenye asili ya Somalia anayewakilisha jimbo la Minnesota katika Baraza la Wawakilishi Marekani amesema, kiwango cha machafuko ya kutumia silaha moto katika jimbo hilo ni kikubwa zaidi kuliko cha kwenye kambi ya wakimbizi Wasomali aliyokuwa akiishi zama za utotoni. Ilhan Omar ambaye alikuwa akihutubia hadhara ya watu wa jimbo lake kuhusiana na machafuko…