
Wapalestina wapata ushindi mwingine Umoja wa Mataifa
Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa imepasisha azimio ikitambua haki ya watu wa Palestina ya kuamua hatima yao wenyewe. Rasimu ya azimio hilo iliwasilishwa na Misri ikishirikiana na serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina katika Umoja wa Mataifa, kwa niaba ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC)….

Indhari ya UNRWA kuhusu kuongezeka umaskini miongoni mwa wakimbizi wa Kipalestina
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) limetahadharisha kuhusu kuongezeka kwa kiasi kikubwa umaskini miongoni mwa wakimbizi wa Kipalestina huko Syria, Lebanon na Ukanda wa Ghaza. Wapalestina zaidi ya milioni 6 wanaishi kama wakimbizi katika nchi mbalimbali na hasa katika nchi zinazopakana na Palestina. Wakimbizi hao wa Kipalestina ambao kabla ya…

Jeshi la Israel lampiga risasi na kumuua shahidi binti wa Kipalestina
Wanajeshi makatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamemuua shahidi msichana wa Kipalestina aliyekuwa na umri wa miaka 19 katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Vyombo vya habari vya Palestina vimeripoti habari hiyo na kueleza kuwa, binti huyo aliyetambuliwa kwa jina la Sana Al-Tal, ameuawa shahidi kwa kumiminiwa risasi na askari wa utawala…

Hamas yasisitiza kutekeleza Tangazo la Algeria na kuhitimisha hitilafu za ndani
Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesisitiza kuwa harakati hiyo ipo tayari kutekeleza Tangazo la Algeria kuhusu mapatano ya kitaifa na kuhitimisha hitilafu za ndani. Abu Marzouq amesisitiza kuwa, Hamas ina hamu na iko tayari ili kuhakikisha kuwa umoja wa kitaifa unapatikana na Tangazo la Algeria linatekelezwa. Amesema, marhala ya sasa…

Wazayuni wakasirishwa na uamuzi wa Umoja wa Mataifa wenye maslahi na Wapalestina
Kamati ya Kupambana na Ukoloni ya Umoja wa Mataifa imepasisha muswada wa Kipalestina ambao ndani yake unataka rai na maoni ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuhusiana na hatua ya utawala wa Kizayuni wa israel ya kuendelea kuikalia kwa mabavu Palestina. Azimio hilo ambalo limepasishwa katika makao makuuu ya Umoja wa Mataifa mjini New…

Utawala wa Kizayuni wakataa kukabidhi maiti za Wapalestina 10 waliouawa shahidi
Kamati inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa utawala huo ghasibu unaendelea kuzuia viwiliwili vya Wapalestina kumi waliouawa shahidi. Kwa mujibu wa chaneli ya habari ya Quds Al-Akhbariya, Kamati ya Wafungwa wa Palestina imetangaza katika taarifa yake siku ya Alkhamisi kwamba Wapalestina hao waliuawa shahidi wakati…

Ripoti: Tel Aviv inatumia “mbinu za kimafia” dhidi ya makundi ya haki za binadamu ya Palestina
Shirika la kutetea haki za binadamu la Palestina limesema katika ripoti yake kwa kamati ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa kwamba Israel inatumia vitisho na mbinu za kimafia kuyanyamazisha mashirika ya kutetea haki za binadamu. Kundi la wanaharakati wa haki za binadamu wa Palestina limeiambia kamati ya Umoja wa Mataifa kwamba katika fremu ya unyanyasaji…

Kiongozi wa HAMAS: Mazingira ya Ukingo wa Magharibi ni utangulizi wa kuutokomeza utawala wa Kizayuni
Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema mazingira ya hivi sasa katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan ni utangulizi wa kutokomezwa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel. Mahmoud Az-Zahar ameongeza kuwa, nchi kama Syria, Lebanon na Palestina ambazo zimedhuriwa na utawala wa Kizayuni, inapasa zisimame pamoja…