
Kiongozi wa Kishia Bahrain: Kuchomwa moto Qur’ani hakuna uhusiano wowote na uhuru wa maoni
Kiongozi wa Waislamu wa Madhehebu ya Shia nchini Bahrain Sheikh Isa Qassim amelaani vikali kitendo cha kuchomwa moto Qur’ani Tukufu hivi karibuni katika nchi za Ulaya. Sheikh Qassim amesema katika taarifa yake kwamba, “Kitendo cha kuvunjia heshima Qur’ani Tukufu kilichotekelezwa na mtu mwenye msimamo mkali, anayejulikana kama Rasmus Paludan – kiongozi wa Chama cha Stram…

Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani ya Iran yaonyesha vipawa
Washindani wanaendelea kuonyesha vipaji vyao katika duru ya mwisho ya toleo la 45 la Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Katika kipindi Ijumaa asubuhi kulikuwa na mashindano ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu nzima. Saeed Aliakbari kutoka Mkoa wa Qazvin alikuwa wa kwanza kujibu maswali ya jopo la waamuzi. Washiriki wengine…

Mashindano ya Qur’ani ya Bint Maktoum Yamalizika
Toleo la 23 la Mashindano ya Qur’ani Tukufu ya Sheikha Hind Bint Maktoum yalimalizika katika Umoja wa Falme za Kiarabu siku ya Alhamisi. Katika siku ya mwisho ya mashindano, wanaume 9 walishindana katika Ukumbi wa Tuzo la Kimataifa la Tuzo la Qur’ani Tukufu la Dubai (DIHQA) katika wilaya ya Al Mamzar ya Dubai, na wanawake…

Tahadhari kuhusu nakala za Qur’ani Tukufu zilizopotoshwa katika intaneti
Waislamu wametakiwa kuchukua tahadhari kuhusu nakala za Qur’ani Tukufu zilizo katika mitandao ya intaneti na aplikesheni kwani imebainika kuwa baadhi zimepotoshwa kwa makusudi. Jumuiya ya Kiislamu Duniani imetoa taarifa na kutangaza kuwepo nakala za Qur’ani Tukufu zenye makosa na potofu kwenye baadhi ya tovuti zisizojulikana na kusema kwamba wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kuwa na msimamo…