#somalia

Magaidi 17 wa al-Shabaab wauwa katika operesheni mpya Somalia

Magaidi 17 wa al-Shabaab wauwa katika operesheni mpya Somalia

Vyombo vya intelejensia vya Somalia vikishirikiana na vya kimataifa vimeangamiza wanachama 17 wa kundi la kigaidi la al-Shabaab. Kwa mujibu wa Wizara ya Habari ya Somalia, magaidi hao waliuawa katika operesheni ya usiku wa kuamkia jana katika mji wa Hawadley, yapata kilomita 40 kaskazini mwa Mogadishu. Taarifa ya wizara hiyo imesema: Operesheni hiyo ilifanywa na…

Jeshi la Somalia: Wanamgambo 18 wa kundi la kigaidi la al-Shabab wamepelekwa jongomeo

Jeshi la Somalia: Wanamgambo 18 wa kundi la kigaidi la al-Shabab wamepelekwa jongomeo

Jeshi la Somalia limetangaza kuwa, limewaangamiza wanachama 18 wa kundi la kigaidi la a-Shabab lenye mfungamano na mtandao wa al-Qaeda. Hayo yameelezwa na Brigedia Jenerali Odowaa Yusuf Rageh Mkuu wa jeshi la Somalia  ambaye amebainisha kuwa, magaidi hao wameuawa katikati ya nchi baada ya kutokea mapigano makali kati yao na jeshi. Aidha amesema kuwa, jeshi la Somalia…

Magaidi wa al Shabab waua raia wasiopungua 18 na kuchoma moto malori ya chakula katikati ya Somalia

Magaidi wa al Shabab waua raia wasiopungua 18 na kuchoma moto malori ya chakula katikati ya Somalia

Genge la kigaidi na ukufurishaji la al Shabab limeua raia wasiopungua 18 katika eneo la Hiran la katikati mwa Somalia na kuteketeza kwa moto malori yaliyokuwa yamesheheni chakula kwa ajili ya watu wenye njaa wa eneo hilo. Genge hilo lenye silaha lilianzisha mashambulizi katika eneo la Hiran katika jimbo la Hirshabelle la katikati mwa Somalia…

Watu 20 wauawa Somalia katika shambulio la kigaidi la al-Shabab

Watu 20 wauawa Somalia katika shambulio la kigaidi la al-Shabab

Watu wasiopungua 20 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia shambulio la kigaidi la al-Shabab katikati mwa Somalia. Duru za usalama zinasema kuwa, shambulio hilo la al-Shabab lililolenga mabasi kadhaa katika mji wa Hiran katikati mwa Somalia limetokea Jumamosi ya leo na kwamba, wanawake na watoto ni miongoni mwa waliouawa katika shambulio hilo. Taarifa zaidi…

Zaidi ya maafisa 8,000 wa polisi wa Somalia wapewa mafunzo na kikosi cha AU

Zaidi ya maafisa 8,000 wa polisi wa Somalia wapewa mafunzo na kikosi cha AU

Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia kimetoa mafunzo na ushauri wa kiusalama kwa maafisa polisi 8,167 wa Somalia kikosi hicho kilipotumwa kwa mara ya kwanza nchini humo mwaka 2009. Mkuu wa Polisi wa Kikosi cha Mpito cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (ATMIS), Rex Dundun amesema hayo na kuongeza kuwa, maafisa…

Rais wa Somalia atangaza vita dhidi ya kundi la al-Shabab, aahidi kulitokomeza

Rais wa Somalia atangaza vita dhidi ya kundi la al-Shabab, aahidi kulitokomeza

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud ametangaza vita dhidi ya kundi la kigaidi la wanamgambo wa al-Shabab ambalpo limekuwa likifanya mashambulio na mauaji mara kwa mara katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika. Rais huyo mpya wa Somalia ameahidi vita vikali vya kutokomeza kundi la al-Shabab katika taarifa yake ya kwanza kwa taifa tangu wanamgambo…

Jinai mpya ya Marekani Somalia, Biden ameua Wasomali 465

Jinai mpya ya Marekani Somalia, Biden ameua Wasomali 465

Shirika linalochunguza mashambulizi ya anga ya kimataifa limefichua kuwa Marekani inaficha idadi halisi ya vifo vya raia nchini Somalia na kwamba idadi ya waliopoteza maisha katika nchi hiyo ya Afrika ni mara 30 zaidi ya ile iliyotangazwa na Pentagon. Kwa mujibu wa taarifa ya tovuti ya “Truthout”, mashambulizi ya anga ya Marekani nchini Somalia katika…

Watu 10 wauawa Mogadishu katika shambulio la magaidi wa al-Shabab

Watu 10 wauawa Mogadishu katika shambulio la magaidi wa al-Shabab

Kwa akkali watu 10 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu kufuatia hujuma na mashambulio ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la al-Shabab. Maafisa wa usalama wanasema kuwa, watu hao 10 wameuawa baada ya wanamgambo wa al-Shabab kuvamia hoteli moja katika mji mkuu Mogadishu. Vyombo vya uusaama vinasema washambuliaji walilipua vilipuzi…