Watu 3 wamejeruhiwa kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea kaskazini mwa Tel Aviv

Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni vimeripoti kutokea mlipuko mkubwa katika eneo la viwanda katika mji wa Hasharon, ulioko kaskazini mwa Tel Aviv, na watu 3 kujeruhiwa katika mlipuko huo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni na mashahidi waliojionea, mlipuko huu ulitokea katika warsha ya kemikali katika eneo la viwanda katika mji wa Ramat Hasharon, ulioko kaskazini mwa Tel Aviv, na moto uliosababishwa na mlipuko huu unaenea. Walisisitiza kuwa sauti ya mlipuko huu ilisikika umbali wa kilomita kumi.

Kulingana na ripoti hii, watu 3 walijeruhiwa katika mlipuko huu.

Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni viliutaja mlipuko huo kuwa ni mkubwa na wa kutisha. Mamlaka ya utawala wa Kizayuni iliwataka wakaazi waliokuwa wakiishi katika eneo la mlipuko huo kufunga madirisha ili kuzuia kupenya kwa gesi hatari.

Magari ya kubebea wagonjwa yamekimbilia eneo la ajali kutoka pande zote.

Mamlaka za utawala wa Kizayuni bado hazijazungumzia sababu za mlipuko huo. Wakati huo huo, habari inaelezea juu ya udhibiti wa moto katika sehemu fulani za warsha hii.

Previous Post
Next Post

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *